Spiritual Healing
Ukiwa unatembea, umekaa, umefanya udhu au hata bila udhu,
endelea kufanya kumsifu Allah kwa maneno hayai ya:
وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى
الْكَعْبَيْنِ
Wamsahoo Bi Ru'oosikum Wa Arjulikum Ilal-Ka‘bayn
Maumivu yatakapoondoka, acha kumsifu
Allah kwa maneno haya hiyo.
Kabla ya kuchomoza kwa jua, mketishe mgonjwa kwa
kuchutama huku uso wake ukiwa umeelekea mashariki.
Mwambie aweke mkono wake wa kulia juu ya upande wa
kichwa unaouma.
Mtoto mwenye umri wa miaka kumi (10) hadi kumi na
miwili (12) asome:
بِسْمِ اللّٰهِ الرَّحْمٰنِ الرَّحِيمِ فَرِيقٌ
كَذَّبْتَ مُهَيْمْ
Bismillahir-Rahmaanir-Raheem Fareequn Kadh-dhabta Muhaym
kisha ampulizie mgonjwa.
Ugonjwa huu huwapata zaidi watoto wadogo.
Katika ugonjwa huu, viumbe wadogo sana wasioweza
kuonekana hata kwa hadubini huzaliana kwa kasi kubwa ndani ya njia ya hewa
kiasi kwamba ndani ya saa chache njia ya kupumua inaweza kuziba.
Usipochukuliwa hatua kwa wakati, viumbe hao huunda
utando unaoziba kabisa njia ya hewa na mgonjwa anaweza kukosa pumzi.
Kwa ajili ya kuondokana na ugonjwa huu hatari, soma
mara moja:
مَنْ ذَا الَّذِيْ يَشْفَعُ عِنْدَهُ إِلَّا بِإِذْنِهِ
Man Dhal-Ladhee Yashfa'u 'Indahu Illaa Bi Idhnih
kisha pulizia ndani ya maji.
Maji hayo yamiminiwe mara kwa mara kooni mwa mgonjwa
huku ukisugua koo kwa upole ili maji yashuke.
Usiwe mzembe katika ugonjwa huu, kwa sababu ni ugonjwa
hatari.
Ikiwa ladha ya chakula imeharibika na kila kitu
kinaonekana kuwa kichungu au kisicho na ladha, basi kabla ya kuchomoza kwa jua,
ukiwa bado hujala chochote, soma kimoyomoyo:
اَلسِّنِّ بِالسِّنِّ
As-Sinni Bis-Sinni
Kisha pulizia ndani ya maji.
Ukiwa umeelekea mashariki, kunywa maji hayo kwa
mafundo matatu (3).